MWENYEKITIN WA CCM, RAIS KIKWETE AFANYA KIKAO MUHIMU NA WABUNGE WA CCM LEO MJINI DODOMA

Sunday, May 19, 2013

 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiwasili ukumbini wakati wa kikao chake na wabunge wa CCM, leo Mei 19, 2013, katika ukumbi wa jengo la White House, Makao Makuu ya CCM, mjini Dodoma. Wengine kushoto ni Spika wa Bunge Anna Makinda, Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenista Mhagama na Mwenyekiti wa Wabunge wa CCM, Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akizungumza wakati wa kikao chake na wabunge wa CCM, leo Mei 19, 2013, katika ukumbi wa jengo la White House, Makao Makuu ya CCM, mjini Dodoma. Wengine kushoto ni Spika wa Bunge Anna Makinda, Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenista Mhagama na Mwenyekiti wa Wabunge wa CCM, Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula.
  Wabunge wa CCM wakiwa kwenye kikao chao na Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete leo kwenye ukumbi wa Jengo la White House, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma.
 Wajumbe kwenye kikao hicho wakibadilishana mawazo ukumbini. Walioketi mbele, Kushoto ni Katibu wa NEC Uchumi na Fedha Zakiah Meghji na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na kulia ni Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migoiro na Mbunge wa Urambo na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta.
  Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara) Mwigulu Nchemba akibadilishana mawazo na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Zanzibar) Vuai Ali Vuai na Katibu wa NEC Oganaizesheni Dk. Muhammed Seif Khatib kwenye kikao hicho.
 Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migiro(kulia) akisalimiana na Mbunge wa Viti Maalum Vicky Kamata wakati wa kikao hicho. Kushoto ni Mbunge wa Same Anne Kilango Malecela.
 Mbunge wa Songea na Waziri wa Mambo ya Ndani,Dk. Emmanuel Nchimbi (kushoto) akitaniana kuhusu Uyanga na Simba na Mwenyekiti wa Simba, Mbunge wa Tabora Aden Rage nje ya ukumbi kabla ya kuanza mkutano huo. Kulia ni Mbunge wa Viti Maalum Esther Bulaya.
Mbunge wa Bunga Steven Wasira (kulia) akibadulishana mawazo na wabunge wenzake, Dk. Kamani na Mkullo kabla ya kikao kuanza
Mbunge wa Kinondoni, Iddi Azan (kushoto) akibadilishana mawazo na wabunge wenzake Khamis Kagasheki na Shabiby nje ya ukumbi
Wabunge wakifurahia jambo nje ya ukumbi wakati wa mkutano huo, Kutoka kushoto ni Dk. Mary Mwanjelwa,  Ritha Kabati, Angela Kairuki, Beatrice Shelukindo na Vicky Kamata
Shabiby akizungumza na Angela Kairuki
Vicky Kamata na Ana Kilango Malecela ukumbini
Dk. Asha-Rose Migiro akimsalimia Mama Anna Kilango Malecela
Dk Maua Daftari na Samiah Suluhu ukumbini
Job Ndugai akimpongeza Mbunge wa Igunga Dk. Dalaly Peter Kafumu kurejeshewa Ubunge
Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro akimsalimia Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa wakati wa kikao hicho cha Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete na wabunge wa CCM
Mbunge wa Kyela Dk. Harrison Mwakyembe akimsikiliza kwa makini Mbunge mwenzake Innocent Kalogeris  wakati wa mkutano huo. Picha zote na BASHIR NKOROMO

RAIS KIKWETE AZINDUA KAMPENI YA LISHE LEO

Thursday, May 16, 2013

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Naibu Waziri wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid akisalimiana  kitabu cha kampeni ya Lishe Tanzania baada ya kukizindua leo Machi 16, 2013  katika bustani ya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam. Kulia ni Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na kushoto ni Mama Salma Kikwete akifuatiwa na Mama Maria Nyerere

UNESCO YAENDESHA WARSHA KUHUSU RIPOTI YA HALI YA ELIMU NA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MAADILI NA MAHUSIANO YA KINGONO KWA VIJANA


Mwenyekiti wa TACAIDS Dk. Fatma Mrisho (katikati) akizungumza wakati kufungua warsha siku moja ya mapitio na uhakikisho wa Ripoti ya hali ya Elimu na Huduma za Afya ya uzazi, maadili na mahusiano ya kingono kwa Vijana nchini ambapo warsha hiyo imeshirikisha Taasisi mbalimbali zikiwemo AMREF, UNICEF, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kutoka Tanzania Bara na Visiwani, TGNP, Wizara ya Afya na ustawi wa Jamii na nyinginezo. Kushoto ni Abdoul Coulibaly wa UNESCO na kulia ni Mwezeshaji wa Warsha hiyo kutoka Chuo kishirikishi cha Elimu cha Chuo kikuu cha Dar es Salaam (DUCE) Dr. Kitila Mkumbo.
Mwezeshaji wa Warsha hiyo kutoka Chuo kishirikishi cha Elimu cha Chuo kikuu cha Dar es Salaam (DUCE) Dr. Kitila Mkumbo akitoa mwongozo kwa washiriki wa warsha hiyo ambapo katika majumuisho yalioamuliwa kwenye warsha iliyofanyika leo ya kujadili Ripoti ya hali ya Elimu na Huduma za Afya ya uzazi, maadili na mahusiano ya kingono kwa Vijana nchini yatawasilishwa katika mkutano wa Mawaziri utakaohusisha nchi 21 za Afrika Mashariki na Kusini.
Picha juu na chini ni National Program Officer – HIV & Sexuality Education Mathias Herman kutoka UNESCO akichambua mpango wa majukumu ya nchi za Afrika Mashariki na Kusini na kutoa ufafanuzi wa matokeo ya utafiti wa Ripoti ya hali ya Elimu na Huduma za Afya ya uzazi, maadili na mahusiano ya kingono kwa Vijana nchini ambapo ameongeza kuwa nchi inatakiwa kujipanga kwa kusaidiwa na UNESCO pamoja na washirika kuongoza jitihada za kitaifa ambazo zitawawezesha washirika wakubwa ambao ni vijana kushiriki katika mikakati ya kitaifa itakayowasidia vijana nchini kujua mtazamo wao.
Pichani ni Washirki wakifuatilia uchambuzi wa Ripoti uliokuwa ukiwasilishwa na Mathais Herman kutoka UNESCO.

Mwakilishi kutoka Wizara ya Elimu na Ufundi stadi Bw. Raymond Benedict (kushoto) akikata kujua kuhusu mapitio ya Ripoti ya hali ya Elimu na Huduma za Afya ya uzazi, maadili na mahusiano ya kingono kwa Vijana nchini, huduma zinazotolewa na serikali na nini hatma na vijana wameelewa kwa kiwango gani.
Pichani juu na chini washiriki wa warsha ya siku moja iliyoandaliwa na shirika la UNESCO nchini wakichangia maoni yao.Pichani juu Katikati ni Mwenyekiti wa Asasi ya vijana ya Umoja wa Mataifa (YUNA) Lwidiko Edward akiwakilisha vijana na kulia ni Abdoul Coulibaly wa UNESCO
Picha juu na chini ni Washirki wakiendelea kufuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye warsha ya siku moja ya ya mapitio na uhakikisho wa Ripoti ya hali ya Elimu na Huduma za Afya ya uzazi, maadili na mahusiano ya kingono kwa Vijana nchini iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam na kufunguliwa na Mwenyekiti wa TACAIDS Dk. Fatma Mrisho.

CCM YAWAPONGEZA VIONGOZI WA DINI

Wednesday, May 15, 2013



   Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi iliyokutana jana Mjini Dodoma imeipongeza serikali kwa hatua inayoendelea kuchukua katika kuchunguza chanzo cha tukio la mlipuko wa Bomu uliotokea Kanisani Jijini Arusha.
Bomu hilo lilirushwa Mei Tano mwaka huu wakati wa uzinduzi wa Kanisa la Romani Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi Parokia ya Olisiti na kusababisha vifo vya watu watatu na majeruhi kadhaa.
 Akizungumza leo Jijini Dar es salaam Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi NAPE NNAUYE ameeleza kuwa taarifa hiyo ya serikali iliwasilishwa jana katika kikao hicho na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dokta EMMANUEL NCHIMBI .
 Kufuatia tukio hilo, Kamati Kuu imelaani na imeitaka serikali kuharakisha uchunguzi pamoja na kuongeza kasi ya uchunguzi wa suala hilo sanjari na kutafuta mzizi wa matukio hayo pamoja na kutoa taarifa mara kwa mara kuhusu maendeleo ya uchunguzi wa tukio hilo.
  Hata hivyo Kamati Kuu imewapongeza viongozi wa Madhehebu ya Dini nchini kwa kuweza kuwaelekeza waumini wao kuhusu mlipuko huo na kuweza kusimamia amani na utulivu tangu kutokea kwa tukio hilo.
 Pia Kamati Kuu imewataka viongozi wa kisiasa nchini kuliachia Jeshi la Polisi liendelee na kazi ya upelelezi wa tukio hilo.
Wakati huo huo, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi-CCM, Rais JAKAYA KIKWETE  wiki ijayo anatarajia kukutana na Wabunge wote wa CCM Mjini Dodoma katika kikao cha kazi. Kikao hicho kitakuwa ni cha siku Mbili kuanzia Mei 18 na 19 mwaka huu. Katika kikao hicho, Wabunge watatumia fursa hiyo kutoa maoni yao kuhusu utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010/2015 katika maeneo mbalimbali ikiwemo katika Majimbo yao ya Uchaguzi.
  NAPE amefafanua kuwa Chama Cha Mapinduzi kimekuwa na utaratibu wa kukutana na Wabunge wa Chama hicho ili kujadili masuala yanayohusu nchi likiwemo suala la utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ambalo ndio Dira ya maendeleo ya wananchi.
Pia amesisitiza kuwa kuitishwa kwa kikao hicho hakuna uhusiano na suala la aina yoyote ya kuwawajibisha Wabunge wa CCM kinidhamu bali ni mkutano wa kawaida na wa kazi.
  Mara baada ya kikao hicho cha Wabunge wa CCM, Kamati Kuu ya CCM itakutana kwa siku Mbili Mjini Dodoma kuanzia Mei 20 hadi 21 mwaka huu.


MKURUGENZI WA FES NCHINI AIPONGEZA CCM KWA KUJENGA DEMOKRASIA NCHINI

Monday, May 13, 2013

Mkurugenzi Mkazi wa FES nchini, Rolf Paasch (Kulia)akizungumza na Makamu Mwenyekiti wa CCM -Bara Ndugu Philip Mangula,leo katika ofisi ndogo za CCM Lumumba.
SHIRIKA la Kijerumani la Friedrich Ebert Stiftung (FES), limekipongeza na kukisifu Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwa kuendelea kujenga utawala bora na kujenga amani ya nchi. Akizungumza na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Bara, Philip Mangula,  Mkurugenzi Mkazi wa FES nchini, Rolf Paasch, alisema shirika lake linatambua juhudi na kazi inayofanywa na CCM katika ujenzi wa demokrasia na amani ya Tanzania.
Paasch alisema Tanzania ni nchi muhimu katika historia ya bara la Afrika hususan mchango wake katika ukombozi wa nchi zilizo kusini mwa Afrika, hivyo inapaswa kuwa mfano na kuhifadhi kumbukumbu muhimu za kihistoria kuhusu ukombozi. "Ni mara yangu ya kwanza kuja Tanzania na nafurahi leo kukutana nawe kiongozi wa juu wa CCM, kwa niaba ya FES naahidi kuimarisha na kuedndeleza ushirikiano uliopo baina yetu na CCM na Tanzania kwa jumla," alisema. Kwa Upande wake Mangula, alisema katika kuhakikisha Tanzania inatunza kumbukumbu muhimu za kihistoria za bara la Afrika, kwa makubaliano na nchi zingine za bara hilo zimeamua kutenga eneo maalumu wilayani Bagamoyo kwa ajili ya ujenzi wa kijiji cha kumbukumbu hiyo. Mangula alimwambia mkurungenzi mkazi huyo kuwa tayari eneo hilo limeshapatikana na kwamba mchakato wa hatua zaidi katika kuelekea ujenzi wake kwa kushirikiana na nchi nyingine, unaendelea

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AKUTANA NA MCHUNGAJI DKT. MATHEW BYAMUNGU NA MKEWE IKULU DAR LEO

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Mchungaji Dkt. Mathew Byamungu, wakati akimkaribisha Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Mei 13, 2013 alipofika kwa mazungumzo akiwa ameongozana na mkewe, Je-Ynung. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Mchungaji Dkt. Mathew Byamungu, wakati akimkaribisha Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Mei 13, 2013 alipofika kwa mazungumzo akiwa ameongozana na mkewe, Je-Ynung. Picha na OMR

RAIS KIKWETE AZINDUA JENGO LA SAYANSI KATIKA KITUO CHA TAASISI YA KIMATAIFA YA KILIMO CHA TROPIKI LEO (PICHA ZAIDI)

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais mstaafu  wa Nigeria na Balozi wa heshima wa  IITA Chief Olesegun Obasanjo na Rais Mstaafu wa Tanzania Mzee Benjamin William Mkapa wakizindua rasmi  jengo la sayansi katika kituo cha Taasisi ya Kimataiafa ya Kilimo cha Tropiki (IITA) Mikocheni jijini Dar es salaam leo Mei 13, 2013.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais mstaafu  wa Nigeria na Balozi wa heshima wa  IITA Chief Olesegun Obasanjo na Rais Mstaafu wa Tanzania Mzee Benjamin William Mkapa katika picha ya pamoja na wadau wa maendeleo bnaada ya kuzindua rasmi  jengo la sayansi katika kituo cha Taasisi ya Kimataiafa ya Kilimo cha Tropiki (IITA) Mikocheni jijini Dar es salaam leo Mei 13, 2013.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais mstaafu  wa Nigeria na Balozi wa heshima wa  IITA Chief Olesegun Obasanjo wakisiliza maelezo ya tafiti mbalimbali za mihogo baada ya kuzindua rasmi  jengo la sayansi katika kituo cha Taasisi ya Kimataiafa ya Kilimo cha Tropiki (IITA) Mikocheni jijini Dar es salaam leo Mei 13, 2013.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na akiangalia katika darubini vimelea vya magonjwa ya mihogo vilivyo katika sehemu ya utafiti baada ya kuzindua rasmi  rasmi  jengo la sayansi katika kituo cha Taasisi ya Kimataiafa ya Kilimo cha Tropiki (IITA) Mikocheni jijini Dar es salaam leo Mei 13, 2013.
Rais Mstaafu Mzee Benjamin William Mkapa akiwa na  Balozi wa Marekani nchini Mhe Alfonso E. Lenhardt  pamoja na  Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Mhe. Tonia Kandiero  wakati wa uzinduzi  rasmi  rasmi  jengo la sayansi katika kituo cha Taasisi ya Kimataiafa ya Kilimo cha Tropiki (IITA) Mikocheni jijini Dar es salaam leo Mei 13, 2013.
PICHA NA IKULU