LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Aug 18, 2013

MATUKIO KATIKA MSIBA WA NEMELA MANGULA, MTOTO WA MZEE MANGULA

Viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali wakiwa pamoja kumpa pole Mzee Philip Mangula kwa kufiwa na mwanawe Nemela Mangula.

Baadhi ya waombolezaji mbalimbali katika msiba wa Nemela Mangula wakiwa wamegubikwa na huzuni  wakiwa nyumbani kwa baba wa Marehemu Masaki jijini Dar es salaam.

Mzee Mangula akiwa pamoja na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali waliofika nyumbani kwake kumpa pole kwa kufiwa na Mwanawe.

Akina mama mbalimbali waliojumuika na familia ys Mzee Mangula katika kuomboleza msiba wa Nemela Mangula.
 Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana Taifa Ndugu Mboni Mhita akisaini kitabu cha Maombolezo ya Msiba wa Nemela P. Mangula Mtoto wa Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa Bara Ndugu Mboni Mhita
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa Uchumi na fedha Mama Zakhia Mengi akisaini Kitabu cha  Maombolezo.

Mama Asharose Migiro Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa SUKI akiwa katika maombolezo ya msiba wa Nemela P Mangula

Paul Christian Makonda akisaini Kitabu Cha Maombolezo ya Msiba wa Mtoto wa  Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa Bara Mzee Philip Mangula.



Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mheshimiwa Mecky Sadick akisaini kitabu cha maombolezo ya msiba wa Nemela Mangula mtoto wa Makama Mwenyekiti Bara Mzee Philip Mangula.

Mama Salma Kikwete,Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa akiwa anasaini kitabu cha maombolezo ya msiba wa Nemela.


Baadhi ya waombolezaji katika  msiba wa Nemela Mangula

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages