LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Sep 18, 2014

KINANA AITEKA MANEROMANGO


  • Avuna wanachama wa upinzani
  • Asisitiza wananchi wajiandikishe kwenye mifuko ya afya ya jamii
  • Awaambia watu wa Maneromango kuwa makini na matapeli wa ardhi
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na viongozi wa UWT wa wilaya ya Kisarawe mara baada ya kuwasili kwenye ofisi za CCM wilaya ya Kisarawe.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisalimia wananchi waliojitokeza kwa wingi kwenye mapokezi ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ambaye leo amefanya ziara kwenye wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasalimu wananchi wa wilaya ya Kisarawe waliojitokeza kwenye mapokezi yaliyofanyika kwenye ofisi za CCM wilaya ya Kisarawe.
 Daktari Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Dk.Happiness Ndosi akimkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwenye hospitali ya wilaya ya Kisarawe .
  Daktari Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Dk.Happiness Ndosi akimpa maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa chumba cha kuhifadhia maiti Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwenye hospitali ya wilaya ya Kisarawe .
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwapa pole wagonjwa katika hospitali ya wilaya ya kisarawe ambapo alijionea maendeleo katika kuboresha huduma za kinana mama na watoto.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiweka jiwe la msingi katika Zahanati ya Palaka iliyopo kijiji cha Palaka kata ya Marumbo.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ufyatuaji wa matofali ya ujenzi wa maabara ya shule ya sekondari Gongoni Maneromango
  Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wananchi kwenye uwanja wa Manerumango sokoni ambapo alisisitiza CCM ndio chama pekee kinachozungumzia maendeleo ya mtanzania kwa sasa.
 Wananchi wakifuatilia mkutano huo Maneromango.
 Mkuu wa mkoa wa Pwani Mheshimiwa Mwantumu Mahiza akijibu baadhi ya maswali yaliyoelekezwa kwake wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Maneromango sokoni.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa amekaa na viongozi wengine wa CCM kwenye meza kuu wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika Maneromango sokoni.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisoma kadi ya aliyekuwa Katibu Kata wa Chadema Shaban Juma Some aliyerudi CCM, zaidi ya watu 30 wamejiunga na CCM leo wakitokea CUF na CHADEMA.
Wanachama wapya wakila kiapo kwenye viwanja vya Maneromango Sokoni.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages