LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Sep 18, 2014

KINANA ATINGISHA KISARAWE, AZINDUA MIRADI NA KUHUTUBIA MAMIA YA WANANCHI MANEROMANGO

 Katibu Mkuu wa CCM,Abdulrahman Kinana akihutubia mamia ya wananchi katika Kijiji cha Maneromango, wilayani Kisarawe, leo Septemba 18, 2014, akiwa katika mwendelezo wa ziara yake katika mkoa wa Pwani, kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM, kusikiliza kero za wananchi huku akijadiliana nao njia ya kuzitatua.
 Katibu wa NWC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye, akihutubia mamia ya wananchi katika Kijiji cha Maneromango, wilayani Kisarawe, leo Septemba 18, 2014,kwenye mkutano huo wa Kinana, aliyeko katika mwendelezo wa ziara yake katika mkoa wa Pwani, kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM, kusikiliza kero za wananchi huku akijadiliana nao njia ya kuzitatua.
 Mamia ya wananchi wa Maneromango wakiwa kwenyemkutano huo wa Kinana aliyeko katika mwendelezo wa ziara yake katika mkoa wa Pwani, kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM, kusikiliza kero za wananchi huku akijadiliana nao njia ya kuzitatua.
 Katibu wa CCM mkoa wa Pwani Joyce Masunga akimtambulisha Mbunge wa zamani wa Kisarawe, Athumani Janguo wakati wa mkutano huo, 
Katibu Mkuu wa CCM akitazama ngoma iliyokuwa ikitumbuizwa na  kikundi cha wananchi katika Uwanja wa Soko la Manaromango,kabla ya kuanza mkutano huo.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akisalimia wananchi bada ya kuwasili Ofisi ya CCM Wilaya ya Kisarawe mkoa wa Pwani leo
 Kinana akitambulishwa kwa baadhi ya viongozi wa CCM na UVCCM baada ya kuwasili kwenye Ofisi ya CCM wilaya ya Kisarawe leo, Septemba 18, 2014. Nyuma yake ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye. 
 Kinana akiwasili kwenye Ofisi ya CCM wilaya ya Kisarawe leo, Septemba 18, 2014 alipowasili kuendelea na ziara yake mkoa wa Pwani.
 Kinana akisalimiana na Mbunge wa zamani wa Kisarawe, Mzee Janguo kwenye Ofisi ya CCM wilaya ya Kisarawe.
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa Wodi namba saba ya Wazazi katika Hospitali ya Wilaya ya Kisarawe, leo, Septemba 18, 2014, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM na kusikiliza kero za wananchi huku akijadiliana nao njia za kuzitatua katika mkoa wa Pwani. Kulia niMgaga Mkuu wa hospitali hiyo, Hapines Ndosi.

Mganga Mkuu wa Hospitaliya Wilaya ya Kisarawe Hapines Ndosi, akimuonyesha Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana maeneo muhimu ya wodi hiyo inayojengwa
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimfariji Mkazi wa Kisarawe, Fatuma Khalfan aliyekuwa akisubiri wakati mtoto wake akipatiwa matibabu katikawodi ya Wazazi katika hospitali ya Wilaya ya Kisarawe mkoa wa Pwani, leo,Septemba 18, 2014.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwa na Mbunge wa Kisarawe, Selemani Jafu wakati akikagua shughuli za Hospitali ya wilaya ya Kisarawe mkoa wa Pwani, leo Septemba 18, 2014.
 Wananchi wakishangilia wakati Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akifungua jiwe la Msingi Ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Palaka,katika Kata ya Malumbo,wilaya ya Kisarawe mkoa wa Pwani, leo Septemba 18, 2014.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akifungua jiwe la Msingi Ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Palaka,katika Kata ya Malumbo,wilaya ya Kisarawe mkoa wa Pwani, leo Septemba 18, 2014. Ujenzi wa Zahanati hiyo umepangwa kugharamia sh. milioni 54 hadi kukamilika kwake. 

Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akiwa na Mbunge wa Kisarawe, Selemani Jafu wakati akizungumza na wananchi baada ya kuzindua ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Palaka, Kata ya Malumbo. 
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akishiriki ufyatuaji matofali kwa ajili ya maabara katika shule ya sekondariya Gongoni, Manerumango, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM katika wilaya ya Kisarawe mkoa wa Pwani. 
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akimsaidia Kinana (kulia) kutoa tofali kwenye mashine, wakati wakishiriki kazi ya ufyatuaji matofali kwa aliji ya ujenzi wa maabara kwenye shule hiyo ya sekondari, leo Septemba 18, 2014. Picha zote na Bashir Nkoromo-CCM Blog

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages